
“na kwa yeye kila amwaminiye huhesabiwa haki katika mambo yale yote asiyoweza kuhesabiwa haki kwa torati ya Musa.
Matendo 13:39
Moja wapo ya vitu muhimu tulivyovipokea baada ya kumwamini YESU kama Bwana na mwokozi wa maisha yetu ni haki ya kuitwa mwana wa Mungu. Na kwa sababu hiyo mimi na wewe kama Watoto wa Mungu tunayo haki ya kuwa na afya njema, msaada wa kiuchumi wakati wa nyakati ngumu na hata msaada wa hekima wakati tunapohitajika kufanya maamuzi sahihi katika mazingira magumu. Haki hizi zote zimepatikana kwa kule kumwamini Yesu kama mwokozi wako. Na lengo la hizo haki ni kukuwezesha wewe kuishi maisha ya furaha, mbali na kuonewa na shetani. Kwa hiyo ndugu mpendwa kama haufurahishwi na namna maisha yako yanavyoenenda basi simama katika zamu yako na kudai haki zako, maana ni katika maombi tu unaweza kupata kila kilicho chako, Barikiwa.


